Saturday, 29 July 2017

TEF yalaani kufukuzwa kwa waandishi wa habari mkutano wa chadema


Jukwaa la wahariri Tanzania (TEF) limesema limepokea kwa masikitiko taarifa za kufukuzwa kwa waandishi wa habari wa kituo cha Televisheni cha shirika la Utangazaji la Tanzania (TBC) wakati wakitekeleza wajibu wao katika ofisi za Chadema.
Mwenyekiti wa TEF, Theophil Makunga amesema katika taarifa kwa vyombo vya habari jana kuwa waandishi wa TBC walikwenda kuchukua habari wakijumuika na wenzao wa vyombo vingine, lakini walibaguliwa na kunyimwa haki ya kupata habari.
“Kitendo cha kuwafukuza waandishi hao waliokwenda kwenye mkutano huo uliomhusisha nwanasheria wa chama hicho,Tundu Lissu hakikubaliki kwa kuwa ni ubaguzi ambao mbali na kuwanyima wananchi wanaotazama TBC haki ya kupata habari,” inasema taarifa hiyo.
Taarifa hiyo inasema vitendo vya kuwabughudhi waandishi wa habari havipaswi kupewa nafasi katika nchi kwa kuwa vinawanyima wananchi haki ya kupata taarifa kama ilivyoainishwa kwemye ibara ya 18(d) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Taarifa hiyo inasema TEF haitavumilia watu au taasisi yoyote iwe binafsi au ya umma ambayo itaingilia uhuru wa habari au kuwakwaza waandishi katika kutekeleza wajibu wao.

Source:Mwananchi Newspaper

No comments:

Post a Comment

MAHUSIANO

DALILI ZINAZOONESHA KUWA UPO KATIKA MAHUSIANO YA KIMAPENZI AMBAYO SIO SAHIHI  Sisi sote tunapenda kuwa na furaha pamoja na kupendwa  katik...