FAHAMU
MBINU MBALIMBALI AMBAZO ZITAKUSAIDIA KUDUMU
KATIKA MAHUSIANO YAKO
Mahusiano ni jambo la muhimu sana katika maisha yetu
ya kila siku. Ni muhimu kwa ajili ya furaha, lakini pia ni muhimu kwa ajili ya
maendeleo yetu. Lakini bado, utafiti unaonesha kwamba zaidi ya asilimia 40 ya
ndoa zinaishia kwenye kupeana talaka. Huu ni uthibitisho wa kwamba, mahusiano
si jambo rahisi.
Zifuatazo ni baadhi ya mbinu ambazo zinaweza
kukusaidia kudumu katika mahusiano
1.KUJIFAHAMU
VIZURI
Kabla ya kuingia katika mahusiano, unapaswa kwanza
ujifahamu wewe ni nani ukiwa peke yako, wewe ni nani ukiwa katika mahusiano, na
wewe ni nani ukiwa na watu wengine kwa ujumla. Vile vile unapaswa kufahamu
unahitaji nini na ni nini matarajio yako katika mahusiano
2.KUMUAMINI
MWENZAKO
Mojawapo kati ya mambo ya msingi sana katika
mahusiano ni pamoja na kuaminiana. Unapaswa kumuamini mwenza wako kwani bila
kumuamini, hakuna jambo lolote ambalo linaweza kufanyika. Na kama humuamini
mwenzako, basi mbinu zote ambazo zinafuata hapo chini zitakuwa hazina umuhimu
wowote ule kwako na katika mahusiano yako.
3.MKUBALI MWENZA WAKO
Unapokuwa katika mahusiano, unapaswa kumkubali
mwenza wake vile namna alivyo, kwa mfano, anavyoonekana na kitu anachokifanya ,
na kama ana madhaifu kadhaa ambayo yanaweza kurekebishika, mnaweza kusaidia
kuyarekebisha kwa pamoja. Na pia kama kuna tofauti kadhaa baina yenu, kila mmoja
wenu hana budi kuziheshimu hizo tofauti kwani sio rahisi mkafanana kwa kila
kitu.
4.MFAHAMIANE
VIZURI
Wenza wanapaswa kufahamiana vizuri na kwa undani
zaidi. Unapaswa kufahamu familia ya mwenza wako, asili yao, kufahamu tabia yake,
kufahamu vitu ambavyo mwenzako anavipenda na ambavyo havipendi. Hii itakusaidia
kujua namna ya kuishi nae vizuri ili muweze kuenda sawa na kudumu katika
mahusiano yenu.
5.KUWA
NA MAWASILIANO YA MARA KWA MARA
Ni vema ukajiwekea tabia ya kuwa na mawasiliano ya
mara kwa mara na mwenza wako na ukawa unamjibu simu na meseji zake kwa wakati.
Lakini pia mnaweza kuwa mnawasiliana kupitia hata mitandao ya kijamii kama
inawezekana.
6.NAMNA
AMBAVYO WEWE NA MWENZA WAKO MNASULUHISHA MATATIZO KATIKA MAHUSIANO YENU
Kwanza unapaswa kufahamu kuwa katika mahusiano,
kutofautiana ni jambo la kawaida sana. Usitarajie kuwa na furaha siku zote,
badala yake unapaswa kufahamu kuwa kuna huzuni pia. Wapenzi wanaodumu, hata
wakiwa na hasira, hutafuta namna ya kuwa karibu, na wakishatatua tatizo,
wanasamehe na kusahau kwani hata Utafiti
unaonesha kuwa, wapenzi wanaosuluhisha matatizo yao na kusahau, huwa wanadumu.Na
jambo la msingi zaidi ni kwamba, huwa wanajifunza kupitia zile tofauti ambazo
zinatokea baina yao, jambo ambalo husaidia mahusiano yao kudumu kwa muda mrefu.
7.NAMNA
AMBAVYO MNASAIDIANA KATIKA MATATIZO MBALIMBALI
Moja kati ya mambo ya kudumisha mahusiano, ni pamoja
na kuwa na uwezo wa kuwa pamoja katika matatizo mbalimbali. Unapaswa kujiuliza,
Je, matatizo yako yanakuleta wewe na mwenza wako pamoja au yanawatenganisha?
Mnashirikiana katika matatizo au manashirikiana katika furaha peke yake?Utafiti
unaonesha kuwa wapenzi ambao wanashirikiana katika matatizo, wanajenga
muunganiko mzuri ambao unaweza kudumu.
8.KUWA
NA MALENGO YA PAMOJA
Mkiwa kama wapenzi ambao mnataka kudumu, mnapaswa kuwa
na malengo ya pamoja katika maisha yenu. Mnatakiwa kuishi mkiwa kama “team”,
jambo ambalo litawasaidia katika kufikia malengo ambayo mnakuwa mmejiwekea kwa
pamoja.Lakini mnapaswa kukumbuka kuwa mnapaswa kujiwekea malengo ambayo
yatawasaidia nyinyi wote wawili. Hii itawasaidia sana kutokana na ukweli kwamba
itawahakikishia kuwa mnakuwa na “uelekeo unaofanana” na hata mwisho wa siku
mnaweza kuja kusheherekea kwa pamoja mafanikio ambayo mnakuwa mmeyapata.Uchunguzi
unaonesha kuwa moja kati ya vitu muhimu kwa ajili ya furaha ni kupambana
kutimiza malengo ambayo ni muhimu. Na kwa upande mwingine, moja kati ya vitu
muhimu kwa ajili ya kuwa na mahusiano yenye furaha ni pamoja na kuwa na malengo
ambayo mtajaribu kuyafikia kwa pamoja.
9.KUWA MKWELI NA MUWAZI
Unapaswa kuwa mkweli na muwazi kwa mwenza wako kueleza
namna ambavyo unajisikia au una wasiwasi
au kitu ambacho unakihitaji.
10.KUPEANA
“ SUPPORT”
Kuna namna mbalimbali ambazo wapenzi wanaweza
wakapeana support. Kwa mfano, kupeana support za kihisia kama vile kumsikiliza
mweza wako kama anahitaji kuzungumza na wewe, au ana mawazo au pengine
anahitaji ushauri n.k Pia kumpa ushirikiano wa aina yoyote ambao anakuwa
anauhitaji kutoka kwako, kumpatia taarifa kuhusu mambo mbalimbali kama atakuwa
anahitaji na kadhalika.
11.KUWA
NA FIKRA CHANYA
Tafiti zinaonesha kuwa mara nyingi Wapenzi wanaodumu
katika mahusiano yao huwa wanazingatia katika mambo mazuri yaliyopo katika
mahusiano yao kuliko yale mabaya. Na pia huwa hawawazi mabaya juu ya mahusiano
yao.
12.KUTOKU”PRETEND”
Wapenzi wanaodumu huwa hawa “pretend” katika
mahusiano yao, na badala yake wanakuwa wakweli. Ukizoea kupretend katika
mahusiano yako, basi utashindwa kudumu kwani utajikuta unashindwa kuendelea
kuwepo katika mahusiano hayo baada ya muda fulani.
13.KUMTETEA
MWENZA WAKO
Unapaswa kumlinda mwenza wako dhidi ya mtu au watu
wengine. Kwa mfano, ukimsikia mtu yoyote anaongea neno baya dhidi ya mwenza wako
unapaswa kumtetea mwenza.Hii ni kutokana na ukweli kwamba, aibu ya mwenza wako
ni aibu yako pia, hivyo hauna budi kumtetea kwa namna yoyote ile.
14.KUMFANYIA
SURPRISE PAMOJA NA KUMFANYIA VITU AMBAVYO YEYE ANAVIPENDA
Unapaswa kumfanyia surprise mwenza wako hata kama ni
mara moja moja au hata kama zikiwa ni surprise
ndogondogo, na pia kumfanyia vitu ambavyo yeye anavipenda sana. Hii itamfanya
awe na furaha wakati wote
15.KUTENGA
MUDA WA KUWA PAMOJA
Wenza wanapaswa kutenga muda wa kuwa pamoja na
kufurahi pamoja. Kwa mfano, mnaweza mkatenga muda wa kwenda kupata pamoja chakula cha usiku, kuweka muda
wa kutoka out na kadhalika.
16.wenza
wanapokuwa pamoja, hawana budi kuwa wanashikana mikono, wanakumbatiana,
kupigana mabusu, kushikana mabega na mengine kama hayo. Kitaalamu, hii
inasaidia sana katika kupunguza msongo wa mawazo, kuongeza hamasa, na kupunguza
presha.
Kimsingi, mahusiano yenye furaha na yanayodumu huwa
hayatokei tu kutoka sehemu fulani, na badala yake huwa yanatengenezwa. Lakini
pia, mahusiano yenye furaha ni muhimu
kwa ajili ya maisha yetu

No comments:
Post a Comment