Friday, 28 July 2017

MAHUSIANO



FAHAMU MBINU MBALIMBALI AMBAZO ZITAKUSAIDIA KUDUMU 
KATIKA MAHUSIANO YAKO
Mahusiano ni jambo la muhimu sana katika maisha yetu ya kila siku. Ni muhimu kwa ajili ya furaha, lakini pia ni muhimu kwa ajili ya maendeleo yetu. Lakini bado, utafiti unaonesha kwamba zaidi ya asilimia 40 ya ndoa zinaishia kwenye kupeana talaka. Huu ni uthibitisho wa kwamba, mahusiano si jambo rahisi.

Zifuatazo ni baadhi ya mbinu ambazo zinaweza kukusaidia kudumu katika mahusiano

1.KUJIFAHAMU VIZURI
Kabla ya kuingia katika mahusiano, unapaswa kwanza ujifahamu wewe ni nani ukiwa peke yako, wewe ni nani ukiwa katika mahusiano, na wewe ni nani ukiwa na watu wengine kwa ujumla. Vile vile unapaswa kufahamu unahitaji nini na ni nini matarajio yako katika mahusiano
2.KUMUAMINI MWENZAKO
Mojawapo kati ya mambo ya msingi sana katika mahusiano ni pamoja na kuaminiana. Unapaswa kumuamini mwenza wako kwani bila kumuamini, hakuna jambo lolote ambalo linaweza kufanyika. Na kama humuamini mwenzako, basi mbinu zote ambazo zinafuata hapo chini zitakuwa hazina umuhimu wowote ule kwako na katika mahusiano yako.
3.MKUBALI  MWENZA WAKO
Unapokuwa katika mahusiano, unapaswa kumkubali mwenza wake vile namna alivyo, kwa mfano, anavyoonekana na kitu anachokifanya , na kama ana madhaifu kadhaa ambayo yanaweza kurekebishika, mnaweza kusaidia kuyarekebisha kwa pamoja. Na pia kama  kuna tofauti kadhaa baina yenu, kila mmoja wenu hana budi kuziheshimu hizo tofauti kwani sio rahisi mkafanana kwa kila kitu.

4.MFAHAMIANE VIZURI
Wenza wanapaswa kufahamiana vizuri na kwa undani zaidi. Unapaswa kufahamu familia ya mwenza wako, asili yao, kufahamu tabia yake, kufahamu vitu ambavyo mwenzako anavipenda na ambavyo havipendi. Hii itakusaidia kujua namna ya kuishi nae vizuri ili muweze kuenda sawa na kudumu katika mahusiano yenu.
5.KUWA NA MAWASILIANO YA MARA KWA MARA
Ni vema ukajiwekea tabia ya kuwa na mawasiliano ya mara kwa mara na mwenza wako na ukawa unamjibu simu na meseji zake kwa wakati. Lakini pia mnaweza kuwa mnawasiliana kupitia hata mitandao ya kijamii kama inawezekana.
6.NAMNA AMBAVYO WEWE NA MWENZA WAKO MNASULUHISHA MATATIZO KATIKA MAHUSIANO YENU
Kwanza unapaswa kufahamu kuwa katika mahusiano, kutofautiana ni jambo la kawaida sana. Usitarajie kuwa na furaha siku zote, badala yake unapaswa kufahamu kuwa kuna huzuni pia. Wapenzi wanaodumu, hata wakiwa na hasira, hutafuta namna ya kuwa karibu, na wakishatatua tatizo, wanasamehe na kusahau kwani hata  Utafiti unaonesha kuwa, wapenzi wanaosuluhisha matatizo yao na kusahau, huwa wanadumu.Na jambo la msingi zaidi ni kwamba, huwa wanajifunza kupitia zile tofauti ambazo zinatokea baina yao, jambo ambalo husaidia mahusiano yao kudumu kwa muda mrefu.
7.NAMNA AMBAVYO MNASAIDIANA KATIKA MATATIZO MBALIMBALI
Moja kati ya mambo ya kudumisha mahusiano, ni pamoja na kuwa na uwezo wa kuwa pamoja katika matatizo mbalimbali. Unapaswa kujiuliza, Je, matatizo yako yanakuleta wewe na mwenza wako pamoja au yanawatenganisha? Mnashirikiana katika matatizo au manashirikiana katika furaha peke yake?Utafiti unaonesha kuwa wapenzi ambao wanashirikiana katika matatizo, wanajenga muunganiko mzuri ambao unaweza kudumu.
8.KUWA NA MALENGO YA PAMOJA
Mkiwa kama wapenzi ambao mnataka kudumu, mnapaswa kuwa na malengo ya pamoja katika maisha yenu. Mnatakiwa kuishi mkiwa kama “team”, jambo ambalo litawasaidia katika kufikia malengo ambayo mnakuwa mmejiwekea kwa pamoja.Lakini mnapaswa kukumbuka kuwa mnapaswa kujiwekea malengo ambayo yatawasaidia nyinyi wote wawili. Hii itawasaidia sana kutokana na ukweli kwamba itawahakikishia kuwa mnakuwa na “uelekeo unaofanana” na hata mwisho wa siku mnaweza kuja kusheherekea kwa pamoja mafanikio ambayo mnakuwa mmeyapata.Uchunguzi unaonesha kuwa moja kati ya vitu muhimu kwa ajili ya furaha ni kupambana kutimiza malengo ambayo ni muhimu. Na kwa upande mwingine, moja kati ya vitu muhimu kwa ajili ya kuwa na mahusiano yenye furaha ni pamoja na kuwa na malengo ambayo mtajaribu kuyafikia kwa pamoja.
 9.KUWA MKWELI NA MUWAZI
Unapaswa kuwa mkweli na muwazi kwa mwenza wako kueleza namna ambavyo unajisikia au una wasiwasi  au kitu ambacho unakihitaji.
10.KUPEANA “ SUPPORT”
Kuna namna mbalimbali ambazo wapenzi wanaweza wakapeana support. Kwa mfano, kupeana support za kihisia kama vile kumsikiliza mweza wako kama anahitaji kuzungumza na wewe, au ana mawazo au pengine anahitaji ushauri n.k Pia kumpa ushirikiano wa aina yoyote ambao anakuwa anauhitaji kutoka kwako, kumpatia taarifa kuhusu mambo mbalimbali kama atakuwa anahitaji na kadhalika.
11.KUWA NA FIKRA CHANYA
Tafiti zinaonesha kuwa mara nyingi Wapenzi wanaodumu katika mahusiano yao huwa wanazingatia katika mambo mazuri yaliyopo katika mahusiano yao kuliko yale mabaya. Na pia huwa hawawazi mabaya juu ya mahusiano yao.
12.KUTOKU”PRETEND”
Wapenzi wanaodumu huwa hawa “pretend” katika mahusiano yao, na badala yake wanakuwa wakweli. Ukizoea kupretend katika mahusiano yako, basi utashindwa kudumu kwani utajikuta unashindwa kuendelea kuwepo katika mahusiano hayo baada ya muda fulani.
13.KUMTETEA  MWENZA WAKO
Unapaswa kumlinda mwenza wako dhidi ya mtu au watu wengine. Kwa mfano, ukimsikia mtu yoyote anaongea neno baya dhidi ya mwenza wako unapaswa kumtetea mwenza.Hii ni kutokana na ukweli kwamba, aibu ya mwenza wako ni aibu yako pia, hivyo hauna budi kumtetea kwa namna yoyote ile.
14.KUMFANYIA SURPRISE PAMOJA NA KUMFANYIA VITU AMBAVYO YEYE ANAVIPENDA
Unapaswa kumfanyia surprise mwenza wako hata kama ni mara moja moja  au hata kama zikiwa ni surprise ndogondogo, na pia kumfanyia vitu ambavyo yeye anavipenda sana. Hii itamfanya awe na furaha wakati wote
15.KUTENGA MUDA WA KUWA PAMOJA
Wenza wanapaswa kutenga muda wa kuwa pamoja na kufurahi pamoja. Kwa mfano, mnaweza mkatenga muda wa kwenda  kupata pamoja chakula cha usiku, kuweka muda wa kutoka out na kadhalika.

16.wenza wanapokuwa pamoja, hawana budi kuwa wanashikana mikono, wanakumbatiana, kupigana mabusu, kushikana mabega na mengine kama hayo. Kitaalamu, hii inasaidia sana katika kupunguza msongo wa mawazo, kuongeza hamasa, na kupunguza presha.


Kimsingi, mahusiano yenye furaha na yanayodumu huwa hayatokei tu kutoka sehemu fulani, na badala yake huwa yanatengenezwa. Lakini pia, mahusiano yenye furaha  ni muhimu kwa ajili ya maisha yetu

No comments:

Post a Comment

MAHUSIANO

DALILI ZINAZOONESHA KUWA UPO KATIKA MAHUSIANO YA KIMAPENZI AMBAYO SIO SAHIHI  Sisi sote tunapenda kuwa na furaha pamoja na kupendwa  katik...